Featured Posts

Friday, May 24, 2013

ANGALIA PICHA ZA AIBU: MUME WA MTU ANASWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI GESTI


INAUMA sana! Wakati wazazi wakihenyeka na wakati mwingine kujinyima ili mabinti zao waweze kupata elimu bora itakayowasaidia maishani mwao wapo wapuuzi wanaokatisha jitihada hizo.
Mwanaume mmoja aitwaye Taliki Juma mkazi wa Temeke – Wailesi jijini Dar es Salaam ameingia  katika  dimbwi la AIBU baada ya kunaswa akiwa na mwanafunzi wa kidato cha pili wakifanya mchezo mchafu.

ANGALIA PICHA ZA MAZISHI YA MWANDISHI MAARUFU WA VITABU NCHINI NIGERIA,CHINUA ACHEBE ALIVYOZIKWA JANA


RIP Chinua Achebe..nakikumbuka kitabu cha 'Things Fall Apart'

Mmoja wa waombelezaji ambaye ni muuzaji wa vitabu hapo Nigeria
Raisi wa Nigeria na Raisi wa Ghana wakiwapungia waombolezaji
Jeneza lilibeba mwili wa marehemu Chinua Achebe

VAN PERSIE AKABIDHIWA KIATU CHAKE CHA DHAHABU

Mshambuliaji wa timu ya manchester united Robin Van Persie Amekabidhiwakiatu cha dhabu akiwa mfungaji bora wa ligi kuu england msimu wa 2012/2013 kwa kufunga magoli 26 Kwa msimu huu.Mchezaji huyo kutoka uholanzi amechukua kiatu hicho msimu wa pili mvululizo ambapo mwaka jana alichukua akiwa anaichezea timu ya arsenal kabla ya kuhamia manchester united msimu huu,

SERIKALI YALAANI VIKALI BUNGE KUDHALILISHWA


Waziri wa Afrika Mashariki Mh Samweli Sitta Akiwa Bungeni leo amelaani vikali gazeti moja kutoka nchi ya jirani kwa kuruhusu picha hapo juu ambayo imelidhalilisha bunge la tanzania.Mh Sitta ametoa kauli hiyo asubuhii wakatia akisoma hotuba ya bajeti ya wizara ya afrika mashariki kwa mwaka 2013/2014.

Mradi wa kuwapatia chakula cha mchana wanafunzi wa skuli ya kusini

 


 
Mradi wa kuwapatia wanafunzi wa Skuli ya Kusini iliyopo Makunduchi waanza rasmi kwa majaribio jana. Akizinduwa rasmi mradi huo mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Kusini, ndugu Faida Khamis Ali (wa tatu kutoka kushoto) aliwataka uongozi wa Skuli ya Kusini kuuenzi mradi huo kwa kutumia fedha za wafadhili kama zilivyokusudiwa.

NAPE ZIARANI UJERUMANI KIKAZI

Nape akisalimiana na baadhi ya viongozi wa SPD kwenye sherehe za miaka 150 ya kuanzishwa kwa chama cha SPD, mjini Leipzig,Ujerumani.

SERIKALI YAWANYOSHEA KIDOLE WANASIASA

Serikali imesema kwamba imebaini kuwa baadhi ya wanasiasa na taasisi za kiraia wanahusika katika kuhamasisha vurugu zinazoendelea mjini Mtwara.
Akitoa kauli ya Serikali bungeni jana, kwa niaba ya Waziri Mkuu, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi alirejea kauli ya Rais Jakaya Kikwete kwamba Serikali itawasaka watu wote wanaohusika na vurugu hizo ndani na nje ya nchi bila kujali umaarufu na madaraka yao.
“Baadhi ya taasisi za kiraia na vyama vya siasa kwa masilahi yao binafsi yasiyo na upeo mpana, vinaweza kudhani kuunga mkono madai ya namna hii ni kuimarisha kukubalika kwao miongoni mwa jamii,” alisema Dk Nchimbi: “Tunawakumbusha msemo wa wahenga usemao ‘tamaa mbele, mauti nyuma’... Tunaapa kuwasaka waasisi wa vurugu ndani na nje ya Mtwara, ndani na nje ya nchi yetu.
Wote waliohusika kupanga, kushawishi, kuandaa na kutekeleza vurugu hizo hawataukwepa mkono wa sheria.”
Alisema Serikali inalaani vikali vurugu hizo akisema wanaozihamasisha “wataipasua nchi, watasababisha vifo vya maelfu ya watu, watajaza taifa vilema na majeruhi na hawatanufaika na matokeo haya mabaya.”

Balozi Seif amtembelea Sheha wa Shehia ya Tomondo kufuatiwa kumwagiwa tindikali

Sheha wa Shehia ya Tomondo Wilaya ya Magharibi Mkoa Mjini Magharibi Bwana Mohd Omar Said { Maarufu Kidevu } akielezea mkasa uliompata wa kumwagiwa Tindi kali { Acid } mbele ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliyefika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja kumfariji.
Picha na Hassan Issa wa –OMPR – ZNZ.
Na Othman Khamis Ame, OMPR
 
Sheha wa Shehia ya Tomondo Wilaya ya Magharibi Bwana Mohd Omar Said { Maarufu Kidevu } anaendelea kupatiwa huduma za matibabu katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja baada ya kumwagiwa Tindi kali { Acid } na mtu asiyejuilikana.
Mkasa huo umempata jana usiku mara baada ya kurejea ibada ya sala ya Isha wakati akiendelea na harakati za kutafuta huduma za maji na kumwagiwa tindi kali hiyo iliyoathiri eneo la kifua chake, Bega pamoja na sehemu za jicho la kulia.
 
Hili ni tukio la tatu kutokea ndani ya koa wa mjini Magharibi likiwahusisha aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Baraza la Manispaa Ndugu Rashid Ali Juma pamoja na Katibu wa Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Fadhil Suleiman Soraga.

Profesa Tibaijuka, NHC wavutana

Waziri Tibaijuka 
Kwa ufupi
Pia Mahakama hiyo iliamuru Li arejeshwe katika makazi hayo, amri ambayo inamaanisha kuondolewa katika nyumba hiyo kwa mpangaji aliyeingizwa badala ya Li ambaye ni Hulstrom aliyekuwa mdaiwa wa pili katika kesi hiyo. Katika kesi hiyo, Li ambaye ni Mtanzania mwenye asili ya China, alikuwa akilalamikia hatua ya kuondolewa kwenye nyumba Nambari 103 iliyopo katika vitalu namba 3, 5, 7 na 8, Barabara ya Haile Selassie, Oysterbay, Dar es Salaam.
Kesi dhidi ya NHC ilifunguliwa mwaka 2006 wakati shirika hilo likiongozwa na Martin Madekwe na imedumu kwa miaka sita hadi Aprili mwaka jana ilipotolewa hukumu wakati shirika hilo likiwa chini ya Nehemia Mchechu aliyeteuliwa mwaka 2010.
Katika hukumu yake ya Aprili 27, 2012, Jaji Atuganile Ngwala aliamuru NHC pamoja na washtakiwa wa pili na wa tatu katika shauri hilo; Lars Eric Hulstrom na Kampuni ya Udalali ya Manyoni, wamlipe Li karibu Sh478 milioni ikiwa ni fidia ya hasara na usumbufu uliosababishwa na kuhamishwa kwake kinyume cha sheria katika nyumba hiyo.
Mchanganuo huo unahusisha Sh70 milioni na Dola za Marekani 177,450 (Sawa na Sh283, 920,000 - Dola moja ni sawa na Sh1,600), gharama za kesi pamoja na riba ambazo pia zinapaswa kulipwa.
Pia Mahakama hiyo iliamuru Li arejeshwe katika makazi hayo, amri ambayo inamaanisha kuondolewa katika nyumba hiyo kwa mpangaji aliyeingizwa badala ya Li ambaye ni Hulstrom aliyekuwa mdaiwa wa pili katika kesi hiyo.

DAKTARI WA MENO KITUO CHA AFYA SABASABA AJINYONGA NA KUFA NDANI YA GESTI MOROGORO

MWILI wa Dk Anold Limo ukiwa katika chumba cha kuifadhia maiti hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro muda mfupi kabla ya mwili huo kuondolea katika nyumba ya kulala wageni ya Camel Nkomola Kihonda baada ya uchun
guzi katika hospitali ya mkoa huo mei 22 mwaka huu.
DAKTARI wa meno Anorld Rimo (umri wa miaka kati ya 30 hadi 40) wa hospitali ya Sabasaba Manispaa ya Morogoro, amekutwa amejinyonga katika nyumba ya kulala wageni ya Camel iliopo Kihonda.

Ujumbe wa TPA watembelea Rwanda.

photoUjumbe wa Mamlaka ya Bandari Tanzania(TPA) uko nchini Rwanda kubadilishana ujuzi na uzoefu na Rwanda kuhusu utekelezaji wa mradi wa kurahisisha na kuwezesha biashara (Trade Facilitation) kwa kutumia TEHAMA – Electronic Single Window System. Muda mfupi ujao TPA itaanza utekelezaji wa mradi huo kwa niaba ya wadau wote wa sekta ya usafirishaji, Forodha, wafanyaniashara na wadau wote wa Tanzania.Ujumbe huo wa Tanzania unaongozwa na Mkuu wa mradi na Kaimu Mkurugenzi wa idara ya TEHAMA-TPA Ndg. Phares Magesa wa kwanza kushoto, wengine ni Mathayo Ntandu, Jesse Shali na Kilian Chale ambao ni maofisa wakuu TPA.

ASKARI WATUHUMIWA KUBAKA NA KUMUUA MJAMZITO MTWARA

Askari wakiwa lindoni/doriani, Mtwara
----------------
Hali ya usalama katika Manispaa ya Mtwara Mikindani mkoani hapa imezidi kuwa mbaya baada ya askari polisi kudaiwa kufanya unyama kwa kuwabaka wanawake na kumpiga risasi mjamzito
Mbali na unyama huo polisi pia wanadaiwa kuchoma moto nyumba tatu za wananchi katika mtaa wa Magomeni na vibanda vya maduka kadhaa na kupora vitu vilivyomo ndani. 
Hata hivyo Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mtwara, Linus Sinzumwa anasema hali ni shwari na kwamba wananchi watoke nje kuendelea na shughuli zao kama kawaida. 
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Ligula, Mohamedi Kodi amethibitisha kupokea mwili wa mjamzito ukiwa na tundu tumboni, zinazoaminika kuwa za risasi na hivyo kufanya idadi ya maiti zilizopokelewa hospitalini hapo kufikia mbili na majeruhi 18:   
“Ni kweli kwa leo( jana) tumepokea maiti moja ya mwanamke ambaye ni mjamzito wa miezi saba, amepigwa risasi tumboni.pia tumepokea mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Chuno, amevunjwa miguu yote kwa risasi.”
Habari zinadai kuwa mjamzito huyo ameuawa akiwa nyumbani kwake baada ya polisi kuvamia makazi yake.
Huduma za kijamii zimesimama, hakuna maduka yaliyo wazi, hakuna usafiri wa daladala wala pikipiki, mji upo kimya, sauti za milio ya mabomu na bunduki zimetawala, wanajeshi waliovalia sare wameuzingira mji wakiwa katika magari na pikipiki. 

MAGAZETI YA LEO IJUMAA TAREHE 24.05.2013

DSC 0113 919d1
DSC 0108 36939
DSC 0111 4ea7b
DSC 0116 1accc

DSC 0109 dd23b
DSC 0110 e1b6f

DSC 0112 e53fb
DSC 0114 fa857
DSC 0115 7d2fb

LAANA: MCHUNGAJI WA 'TAG' KILIMANJARO ATIWA MBARONI KWA KULAZIMISHA PENZI LA KONDOO WAKE BILA KINGA.


KESI ya kutorosha wanafunzi inayomkabili Mchungaji wa Kanisa la Tanzania Assemblies Of God (TAG), Jean Felix Bamana, Raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Jumatatu wiki hii ilianza kurindima katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi, Kilimanjaro huku upande wa walalamikaji ukiiambia korti, ‘mchungaji alitaka penzi bila kinga’.
Mchungaji huyo alitiwa mbaroni


Machi 13, mwaka huu ndani ya Hoteli ya Grand iliyopo Magomeni, Dar akiwa na wanafunzi wawili, watoto wa familia moja, Artha Swai (17) na Angel Swai (19) ambao alidaiwa kuwatorosha kutoka mjini hapa.

Katika kesi ya msingi, mchungaji huyo alidaiwa kuwadanganya watoto hao kwamba alikuwa akiwafanyia mpango wa kwenda kusoma nje ya nchi lakini badala yake aliwaweka hotelini na kumtaka kimapenzi mmoja wao

HATIMAYE DR. SLAA AKUBALIWA KUOANA NA MPENZI WAKE

HATIMAYE Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni, imetupilia mbali rufaa iliyokuwa imekatwa na aliyekuwa mume wa Josephine Mushumbusi( KWA  SASA  NI  MCHUMBA WA DR. SLAA) , Maimbo baada ya kuiona rufaa hiyo haina msingi wowote kisheria.
Hukumu hiyo ya rufaa ya  madai ya ndoa Na.32/2012 ilitolewa leo na Hakimu Aniseth Wambura ambapo alisema mahakama yake imefikia uamuzi huo wa kuitupa rufaa hiyo kwasababu haina mantiki ya kisheria.
Hakimu Wambura alisema mahakama yake imekubalina na hukumu iliyotolewa Aprili 2012 na Mahakama ya Mwanzo Sinza katika kesi ya madai talaka iliyokuwa imefunguliwa na Mushumbusi anayetetewa na wakili wa kujitegemea Philemon Mutakyamilwa  dhidi ya Maimbo ambapo mahakama hiyo ya chini ilitangaza kuwa hakukuwa na ndoa baina ya watu hao kwasababu Maimbo alikuwa ni mzinzi, simwaminifu katika ndoa yake na alikuwa akimtesa mkewe.

POLISI RUVUMA WAKAMATA TENA PEMBE ZA NDOVU

 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Deusdedit Nsimeki akiwaonyesha waandsi wa Habari (Hawapo pichani) Pembe mbili za ndovu miongoni mwa zilizokamatwa zenye Thamani ya  Shilingi milioni 38,893,000. Pembe hizo zote zimekamatwa Kijiji cha Mandepwende  wilayani Namtumbo.

Naye  Kamanda wa Kikosi cha Kuzuia Ujangili Kanda ya Kusini  Abedi Mwari, (Mwenye shati la kiraia) akimuonyesha hesabu kamili ya Pembe zilizopatikan Kamanda Nsimeki (Mwenye Sare ya Polisi) huku waandishi wa habari wakifuatilia tukio hilo  katika Ofisi ya Polisi Mkoa wa Ruvuma leo

ANGALIA PICHA KUTOKA MTWARA JANA KUTOKANA NA VURUGU





Mpaka sasa ni vita baina ya wananchi na maaskari. Mabomu yamesikika pamoja na milio ya risasi masaa 24. Na milio ya Risasi na mabomu inaendelea kusikika.
Raia wapatao 7 wameripotiwa kufariki (wengine walipelekwa hospitali ya Ndanda Ndogo na mmoja ameripotiwa kupokelewa Ligula. 
Nyumba za viongozi zinaendelea kuchomwa moto. 
Majibizano baina ya Polisi na Raia yanaendelea maeneo ya Magomeni, Nkanaledi na Mikindani. 

ANGALIA PICHA YA MAJAMBAZI WAWILI WANUSURIKA KUUAWA MKOANI LINDI

clip_image001Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi,George Mwakajinga akionyesha silaha iliyokutwa kwa majambazi hayo.clip_image001[6]Jeshi la Polisi Mkoani Lindi linawashikilia watu wawili kwa Tuhuma za Unyanganyi kwa kutumia silaha na kujeruhi Mfanyabiasha wa Duka katika kijiji Cha Kitomanga Wilayani Lindi huku wakiwa katika hospital ya Mkoa baada ya kunusurika kufa kufuatia Wananchi wenye hasira kutaka kuwaua kwa kuwachoma Moto.
Akiongea na waandishi wa habari Ofisi kwake hii leo,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi,George Mwakajinga alieleza kuwa Watuhumiwa hao waliojitambulisha kwa Rajabu Juma Mbete(26) mkazi wa manispaa ya Lindi na Hamis Athuman(32) mkazi wa Mbembetini Kibiti Mkoani Pwani licha ya kupora simu 6 na fedha taslim laki 6 pia walimjeruhi kwa Mapanga Bw Hamis Hassan Muuza duka hilo.clip_image001[8]Mwakajinga alibainisha kuwa Majambazi hayo yanayosadikiwa kuwa 4 walifanikiwa kukimbia baada ya Bunduki waliyokuwa nayo kugoma kufyetua risasi hali iliyofanya wanavijiji vya Kitomanga,Mkwajuni na Mbwemkuru kuanza msako na kufanikiwa kuwakamata na kuwajeruhi kwa kuwapiga na kuwachoma moto kabla hawajapata msaada wa Jeshi la Polisi.
Akielezea kuhusu kukutwa na risasi tatu za Shortgun,Bangi pamoja na Bunduki aina ya Shortgun ya kienyeji, Kamanda mwakajinga alifafanua Bunduki hiyo Ambayo hutumia risasi za Short gun pia walikutwa na risasi 3.

ANGALIA PICHA ZA SHEHA WA TOMONDO- ZANZIBAR ALIYEMWAGIWA TINDIKALI J

\
Sheha Mohammed Omary Said aliyemwagiwa tindikali na mtu asiyejulikana akiwa katika hospitali ya Mnazi Mmoja Unguja akipatiwa matibabu, Sheikh Mohammed amepata maumivu makali sehemu za kifuwa na jicho kuumia
Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi,Mukhadam Khamis,amesema chombo kilichotumika kumwagia tindikali Sheha huyo kilipatikana eneo la tukio na kwamba polisi imekichukua kwa kukichunguza kitaalam ili kugundua aliyekuwa akikitumia kwa kuangalia alama za vidole.
Sheha huyo alimwagiwa tindikali jana usiku wakati alipotoka nje ya nyumba yake kuchota maji na ndipo mhalifu huyo alipomwagia tindikali na kwamba hakuweza kumtambua.

BALOZI KAMALA AWEKA SAHIHI HATI YA MAKUBALIANO NA SANEC.

Balozi wa Tanzania BANELUX na Jumuiya ya Ulaya Balozi Dr. Diodorus Buberwa Kamala akiweka sahihi Hati ya Makubaliano na taasisi ya Uholanzi ya SANEC kwa ajili ya SANEC kushirikiana na Ubalozi wa Tanzania BENELUX kutekeleza Sera ya Tanzania ya Diplomasia ya Uchumi. Kushoto ni Bwana Mark Agterdenbosch Meneja Mkuu wa SANEC. Uwekaji sahihi umefanyika leo The Hague Uholanzi.

RAIS KIKWETE AMWAPISHA MWENYEKITI WA TUME YA KUREKEBISHA SHERIA NA MABALOZI WAPYA WANNE

8E9U8078
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal  na Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe wakiwa katika picha ya pamoja na mabalozi wapya waliopaishwa leo ikulu jijini Dar es Salaam.aliyesimama mbele kushoto no Balozi Liberata Mulamula anayekuwa Balozi Mpya wa Tanzania nchini Marekani.Waliosimama nyuma kutoka kushoto ni Balozi mpya wa Tanzania Uholanzi Wilson Masilingi,Balozi mpya wa Tanzania katika visiwa vya Commoro Chabaka Kilumanga,Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania Umoja wa Mataifa Geneva Balozi Modest jonathan Mero na Balozi mpya wa Tanzania katika falme za Kiarabu(UAE)Mbarouk Nassor Mbarouk.Kabla ya uteuzi Balozi Liberata Mulamula alikuwa msaidi wa Rais Masuala ya kidiplomasia na aliwahi kuwa katibu mkuu wa nchi za  Maziwa Makuu.(picha na Freddy Maro)Balozi Kilumanga-Commoro AkiapaBalozi Masilingi-Uholanzi akiapaBalozi Masilingi-Uholanzi akiapaBalozi Mbarouk Nassor Mbarouk (UAE) akiapaBalozi Mbarouk Nassor Mbarouk (UAE) akiapaBalozi Mero-Geneva akiapaBalozi Mero-Geneva akiapaJaji Aloycius Mujuluzi akiapaJaji Aloycius Mujuluzi akiapa

J.K KIKWETE ATHIBITISHIA UMMA KWAMBA PSPF IKO IMARA

12 4d1b3
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa PSPF Ndugu. Adam H. Mayingu tuzo ya kuwa Mfuko wa kwanza wa Hifadhi ya Jamii Tanzania kutoa mikopo ya nyumba kwa wanachama wake. Tuzo hiyo ilitolewa kwenye maadhimisho ya kilele cha Wiki ya Mifuko ya Jamii mjini Dodoma. Mh. Raisi alisema PSPF ni mfuko madhubuti na una fursa nyingi za kimaendeleo kwa wananchi wa Tanzaniai na unauwezo mkubwa na salama katika uwekezaji . Aliongezea kwa kusema sio kweli kwamba Mfuko huu uko mahututi kama ilivyozungumziwa kwenye baadhi ya vyombo vya habari, bali Mfuko huu unadai wadai wake Trilioni 6 na kudai sio kufilisika tena
22 4d38b
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete akisoma kipeperushi cha nyumba za PSPF zinazokopeshwa kwa wanachama wa Mfuko huo, huku akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huo ndugu Adam H. Mayingu akimuelezea kuhusu nyumba hizo na fursa zingine zilizopo PSPF kwa Watanzania ikiwa ni pamoja na ujumbe kwa Watanzania kwamba mtu yeyote mwenye umri usiopungua miaka 18 anaweza kuwa mwanachama wa PSPF

42 161c8
Mtangazaji wa TBC Amina Mollel akikabidhi fomu ya kujiunga na PSPF kwa Meneja Masoko wa Mfuko huo Bi. Costantina Martin mala baada ya kuvutiwa na kukata shauri ya kuwa mwanachama wa Mfuko wa kwa njia ya uchangiaji wa hiari
52 4f257
Timu ya PSPF iliyokuwa kwenye maonyesho ya wiki ya hifadhi ya Jamii wakiwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wao ndugu Adamu Mayingu katikati. Timu hiyo inastahili pongezi kutokana na uduma bora waliyokuwa wakiitoa kwa wananchi waliokuwa wakitembelea banda hilo la PSPF pale Nyerere squire Dodoma.

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 

Test Footer

© Jackson Audiface 2011. All right reserved